• HABARI MPYA

    Thursday, November 09, 2017

    MAFUNZO YA SOKA LA UFUKWENI KUFANYIKA NOVEMBA 18 VYUONI

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) litatoa mafunzo ya soka la ufukweni (Beach Soccer) kwa vyuo mbalimbali hapa nchini vilivyothibitisha kushiriki Ligi Maalumu ya soka la Ufukweni itakayoanza Novemba 18, 2017.
    Kwa upande wa mafunzo ni kwamba yatafanyia siku tano kabla ya kuanza kwa ligi hiyo ambako itakuwa ni Novemba 13, mwaka hu. TFF imepanga kutoa mafunzo hayo kwa vyuo hivyo ili wauelewe zaidi mchezo huo pamoja na sheria zake.
    Tumepeleka mchezo huo kwenye vyuo ili kutoa hamasa ya soka la ufukweni kuenea zaidi na kuweka hazina ya wachezaji wa timu ya taifa.
    Mpaka sasa vyuo 14 tayari vimethibitisha kimaandishi kushiriki kwenye mafunzo hayo.
    Vyuo vilivyothibitisha kushiriki ni Chuo cha Ardhi, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Chuo Cha Ufundi (DIT), Chuo cha Usafirishaji (NIT), Chuo cha Elimu ya Tiba cha Kahiruki, Chuo cha Elimu ya Biashara cha Lisbon, Chuo cha Silva , Chuo UAUT, TIA, El-Maktoum collage Engineering, Magogoni, Chuo cha uandishi wa habari DSJ na TSJ.
    Mafunzo hayo yatatanguliwa na tukio la kukutana na viongozi wa vyuo shiriki hapo Novemba 10, 2017.
    Wakati huo huo kozi ya waamuzi wa Soka la Soka la Ufukweni imeanza leo Novemba 7, 2017 katika Makao Makuu ya TFF Karume, Dar es Salaam ambayo yanatarajiwa kumalizika Novemba 12, 2017.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAFUNZO YA SOKA LA UFUKWENI KUFANYIKA NOVEMBA 18 VYUONI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top