• HABARI MPYA

    Sunday, November 26, 2017

    YANGA NA TANZANIA PRISONS KATIKA PICHA JANA CHAMAZI

    Kiungo wa ulinzi wa Tanzania Prisons, Jumanne Elfadhili (kulia) akinyoosha mguu juu kuokoa dhidi ya kiungo wa Yanga, Emmanuel Martin (katikati) katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya 1-1


    Mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa akimtoka beki wa Tanzania Prisons, Nurdin Chona
    Beki wa Yanga, Gardiel Michael akimuacha chini mchezaji wa Prisons, Salum Kimenya 
    Mshambuliaji wa Prisons, Eliuter Mpepo akimtoka beki wa Yanga, Andrew Vincent 'Dante'
    Beki wa Tanzania Prisons, Michael Ismail akimiliki mpira pembeni ya Gardiel Michael wa Yanga
    Mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajib akiondoka na mpira dhidi ya Eliuter Mpepo wa Prisons 
    Michael Ismail wa Tanzania Prisons akimdhibiti winga wa Yanga, Emmanuel Martin 
    Ibrahim Ajib wa Yanga (kulia) na Salum Kimenya wa Prisons wakinyoosha mikono juu kumuuliza refa nani katoa nje mpira
    Kocha wa Yanga, Mzambia George Lwandamina akiwapa maelekezo wachezaji wake jana 
    Wachezaji wa Tanzania Prisons wakifanya maombi katika lango lao kabla ya mchezo kuanza jana 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA NA TANZANIA PRISONS KATIKA PICHA JANA CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top