// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MADEGA AFARIKI DUNIA BUKOBA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MADEGA AFARIKI DUNIA BUKOBA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, December 16, 2014

    MADEGA AFARIKI DUNIA BUKOBA

    Na Boniface Wambura, DAR ES SALAAM
    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Kocha Mshindo Madega kilichotokea leo (Desemba 16 mwaka huu) mjini Bukoba.
    Mbali ya kuwahi kuwa mchezaji katika timu ya RTC Kagera, Kocha Madega aliwahi kufundisha timu za Kagera Stars, Mwadui na kombaini ya Copa Coca-Cola ya Mkoa wa Kagera.
    Mchango wake katika mchezo wa mpira wa miguu tangu akiwa kocha na baadaye kocha utakumbukwa daima.
    Jama Malinzi kushoto, Rais wa TFF ambayo imepokea kwa masikitiko taaria ya kifo cha kocha Madega 

    Tunatoa salama za rambirambi kwa familia ya marehemu, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA), Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) Mkoa wa Kagera na klabu ya Bukoba Veterans na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo.
    TFF itawakilishwa kwenye msiba huo na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MADEGA AFARIKI DUNIA BUKOBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top