• HABARI MPYA

    Tuesday, March 20, 2012

    WAALGERIA 35 WATUA KESHO DAR


    KIKOSI cha watu 35 cha timu ya ES Setif ya Algeria kinatarajiwa kuwasili nchini  leo saa 12 alfajiri kwa ndege ya EgyptAir kwa ajili ya mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Simba itakayochezwa Machi 25 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Ofisa habari wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura alisema jana kwamba msafara huo unahusisha  wachezaji, benchi la ufundi, viongozi wa timu, kiongozi wa msafara kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu la Algeria (FAF) wakati watatu ni waandishi wa habari.
    Aliwataja wachezaji 20 katika msafara huo ni Mohamed Benhamou, Sofiane Bengorine, Riadh Benchadi, Smain Diss, Farouk Belkaid, Khaled Gourmi, Mourad Delhoum, Said Arroussi, Mokhtar Benmoussa, Tarek Berguiga, Mohamed Aoudi na Amir Karaoui.
    Wengine ni Mohamed El Amine Tiouli, Racid Ferrahi, Youcef Ghezzali, Youssef Sofiane, Mokhtar Megueni, Rachid Nadji, Abderrahmane Hachoud na Akram Djahnit. Kocha wa timu hiyo ni Alain Norbert Geiger ambaye ni raia wa Uswisi.
    Mchezo huu utakaoanza kurindima saa 10 kamili jioni ukichezeshwa na waamuzi kutoka nchini Rwanda  Hudu Munyemana atakayesimama kati akisaidiwa na Felicien Kabanda, Theogene Ndagijimana na Edouard Bahizi, huku kamishna wa mechi hiyo atakuwa  Felix Tangawarima kutoka Zimbabwe.
    Timu hizo zitarejeana Algeria Aprili 6  na iwapo Simba itashinda
    itacheza mechi ya kwanza nyumbani Aprili 29 mwaka huu na mshindi kati ya El Ahly Shandy ya Sudan na Ferroviario de Maputo ya Msumbiji ambapoya marudiano itachezwa kati ya Mei 11, 12 na 13 mwaka huu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAALGERIA 35 WATUA KESHO DAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top