• HABARI MPYA

    Thursday, March 29, 2012

    KIBERA ACHA CHUKI YA KASONGO MPINDA NA MK GROUP


    Kasongo Mpinda

    WIMBO:-KIBERA ACHA CHUKI
    MTUNZI:-KASONGO MPINDA.”CRYTON”
    WAIMBAJI:-KASONGO MPINDA.
    BENDI:-MK GROUP.”NGULUPA TUPATUPA DANCE”
    KATIKA wimbo huu mbali na ujumbe unaotuasa jamii kuondokana na roha za fihi na chuki huku ukituelekeza kuondokana na ubinafsi bali maisha yetu yanastahili kutawaliwa na upendo; utamkubali mwana mama;Asia Daruweshi kwa jinsi alivyomudu kucheza na kinanda kwa umahili mkubwa.
    Ama utaridhika na sauti yenye msisitizo katika ghani ya mtunzi wa kibao hiki; Nguli Kasongo Mpinda”Cryton”kwa jinsi alivyoichezea kwa kupanda na kushuka huku akiwasilisha Ujumbe endelevu tofauti na vibao vya watunzi wa leo hii hususani wa kizazi kipya ambapo nyimbo zao nyingi hazina maudhui, na pindi upatikanapo basi huwa hasi.
    Mtunzi na Mwimbaji anamkanya muhusika kuondokana na tabia aliyonayo ambayo haina maslahi hapa duniani. Kwani yastahili UCHEKE NA WATU UPATE VIATU. Kinyume na hapo, tabia aliyonayo ya ubinafsi,chuki na roho mbaya atendayo itamletea madhara hapa duniani naaam PELE NDILO LIWALO DONDA!
    Tunakumbushwa kwamba sisi sote ni bin Adamu,yatupasa tupendane asilani tusiwekeane kinyongo.yastahili tusaidizane kwa kila jambo,pindi unapomuona mwenzio yumo kwenye kisima kirefu mpe mkono umvute na si kumnyanyapaa kwa ugumu wa maisha yanayomkabili.
    Tungo hii iliyorekodiwa mnamo mwaka 1986,imefanyiwa kazi inavyostahili na kuleta mvuto kwa msikilizaji,mbali na mtunzi pamoja na “Super Mama;”Asia Daruweshi ni Andy Swebe aliyeungurumisha gitaa zito, Mafumu Bilali “Super Sax”ama Bombenga aliyepuliza Saxaphone, Joseph Mulenga “King Spoiler” aliyepiga gitaa linaloongoza na Monga Stanley”Monga Stan”aliyecheza na gitaa la kati “Rythym;
    Trampet zilipulizwa na Abdallha Tuba na Kayembe Ndalambo,huku Abdallha Rock akikaanga chipsi”Drums”na Tumba  zikiwa katika  himaya za Sidy Moris”Super Conga”

    SASA IMBA:-
    Mpende mwenzioo
    Kama unavyojipenda wewee eeeh!
    Mwenye upendoo
    Hana Hasiraa
    Mwenye upendoo ni mtulivuu
    Mwenye upendoo huwatumikia wenzakee
    Upendo ni utumishi
    Utumishi ni upendo
    Upendo ni uhai
    Chuki ni mauti
    Upendo wa kwelii
    Sio wa maneno matupu maamaaaa
    Mbali na matendo maamaaaa
    Mbali na matendooooo oooh!
    {Wee Kiberaa Acha chuki wee..utaleta ugomvi eee}
    Mpende mwenzioo
    Kama unavyojipenda wewee eeeh!
    Mwenye upendoo
    Hana Hasiraa
    Mwenye upendoo ni mtulivuu
    Mwenye upendoo huwatumikia wenzakee
    Upendo ni utumishi
    Utumishi ni upendo
    Upendo ni uhai
    Chuki ni mauti
    Upendo wa kwelii
    Sio wa maneno matupu maamaaaa
    Mbali na matendo maamaaaa
    Mbali na matendooooo oooh!

    CHORUS:-
    Kibera acha chuki eee
    Chuki yaleta uchawii yeeh..
    Kibera acha chuki eee
    Chuki yaleta migonganoo oooh..
    Kibera acha chuki eeeeh…
    Chuki yavunja umoja yeeeh..yooo…Kiberaaa!
    Kibera weee bwana Kiberaaa
    Ooooo..  yeee Kiberaa
    Kibera wacha weee Kiberaaa  aaaah!
    Kibera acha chuki eee
    Chuki yaleta ugomvii yeeh..
    Kibera acha chuki eee
    Chuki yaleta migonganoo oooh..
    Kibera acha chuki eeeeh…
    Chuki yavunja umoja yeeeh..yooo…Kiberaaa!
    Kibera weee bwana Kiberaaa
    Ooooo..  yeee Kiberaa
    Kibera wacha weee Kiberaaa  aaaah!
    Oooo…yooo Kiberaaaa
    Kibera wee bwana Kiberaa…
    Oooo…yeeeh Kiberaa
    Kibera wacha wee Kiberaaaah!

    Kibera acha chuki eee
    Chuki yaleta uchawii yeeh..
    Kibera acha chuki eee
    Chuki yaleta migonganoo oooh..
    Kibera acha chuki eeeeh…
    Chuki yavunja umoja yeeeh..yooo…Kiberaaa!
    Kibera weee bwana Kiberaaa
    Ooooo..  yeee Kiberaa
    Kibera wacha weee Kiberaaa  aaaah!
    Oooo…yoooh Kiberaa
    Kiberaa wee bwana Kiberaaa
    Ooo… yeeeh Kiberaaa
    Kiberaa wacha wee Kiberaaa
    Oooo… yooo Kiberaaa
    Kiberaa weee bwana Kiberaaaaa
    Aaaa Ngulupaaa Ngulupaaa
    Aaaaa Ngulupaaa Ngulupaaaa
    Aaaa Ngulupaaa Ngulupaaa
    Ngulupaaa Ngulupaaa
    Ngulupaaa Ngulupaaaa
    Ooooo..  yeee Kiberaa
    Kibwacha weee Kiberaaa  aaaah!
    Oooo…yoooh Kiberaa
    Kiberaa wee bwana Kiberaaa
    Ooo… yeeeh Kiberaaa
    Kiberaa wacha wee Kiberaaa
    Oooo… yooo Kiberaaa
    Kiberaa weee bwana Kiberaaaaa
    Ooooo..  yeee Kiberaa
    Kibera wacha weee Kiberaaa  aaaah!
    Oooo…yoooh
    Ooooo..  yeee Kiberaa
    Kibera wacha weee Kiberaaa  aaaah!
    Oooo…yoooh Kiberaa
    Kiberaa wee bwana Kiberaaa
    Ooo… yeeeh Kiberaaa
    Kiberaa wacha wee Kiberaaa
    Oooo… yooo Kiberaaa
    Kiberaa weee bwana Kiberaaaaa
    Kiberaa
    Kiberaa wee bwana Kiberaaa
    Ooo… yeeeh Kiberaaa
    Kiberaa wacha wee Kiberaaa
    Oooo… yooo Kiberaaa
    Kiberaa weee bwana Kiberaaaaa
    Ooooo..  yeee Kiberaa
    Kibera wacha weee Kiberaaa  aaaah!
    Oooo…yoooh Kiberaa
    Kiberaa wee bwana Kiberaaa
    Ooo… yeeeh Kiberaaa
    Kiberaa wacha wee Kiberaaa
    Oooo… yooo Kiberaaa
    Kiberaa weee bwana Kiberaaaaa

    (IMEANDALIWA NA ALLY LITYAWI)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIBERA ACHA CHUKI YA KASONGO MPINDA NA MK GROUP Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top