• HABARI MPYA

    Tuesday, March 27, 2012

    BIBI CHEKA KUTAMBULISHWA MOROGORO

    Bibi Cheka akiimba kwenye Media Day Bonanza Jumamosi
    KUNDI la TMK Wanaume Family, limeandaa shoo maalum ya kumtambulisha mwanamuziki chupukizi, lakini aliyekula chumvi, Bibi Cheka ambalo litafanyika mkoani Morogoro Aprili 8, mwaka huu.
    Said Fela, bosi wa TMK Wanaume Family alisema shoo hilo litajulikana kama Mkubwa na Wanawe na wasanii wengine watakaosindikiza shoo hilo Mh Temba, Ferooz, Easy Man, Nurdin, Shilole, Kanga Moko, Mugogo na Dogo Muu.
    Fela alisema kwamba siku hiyo, Dogo Muu atatoa zawadi ya TV ya inchi 21 kwa dogo atakayeimba vizuri wimbo wa Naenda Kusema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BIBI CHEKA KUTAMBULISHWA MOROGORO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top