• HABARI MPYA

    Tuesday, March 27, 2012

    RAIS FIFA HALI BADO MBAYA

    Havelange
    RAIS wa zamani wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Joao Havelange ameingia katika wiki ya pili tangu alazwe katika hospitali ya Samaritano na yuko katika hali mbaya kwa sababu ya madhara yanayomsibu kwenye kifundo cha mguu wake wa kulia.
    Taarifa ya hospital ya Samaritano imesema juana kwamba babu huyo mwenye umri wa miaka 95 sasa, Havelange anatibiwa kwa dawa za antibiotics na afya kwa hakika si njema.
    Havelange alilazwa Machi 18 kutokabna na matatizo yake hiyo yanayosababisha kudhoofu kwa kiungo, ingawa anapumua bila msaada wa mashine.
    Alistaafu kwenye Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki mwaka jana,  kwa sababu za kiafya. Havelange alikuwa rais wa FIFA tangu 1974-98.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RAIS FIFA HALI BADO MBAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top