KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’ ,
Charles Boniface Mkwasa ametaja kikosi cha wachezaji 25 ambacho kitaingia
kambini Machi 25 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya program yake ya maandalizi kabla
ya mechi dhidi ya Ethiopia.
Ofisa habari wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) alisema jana kwamba kambi hiyo itakayokuwa ya
muda mfupi itamuwezesha kocha huyo kuchagua wachezaji anaoona watafaa
kuitumikia timu hiyo katika michezo hiyo.
Wachezaji hao ni pamoja na Amina Salum (Lord Baden Sekondari,
Pwani), Asha Rashid (Mburahati Queens), Aziza Mwadini (New Generation,
Zanzibar), Esther Mayala (Street Girls, Mwanza), Evelyn Senkubo (Mburahati
Queens), Fadhila Hamad (Uzuri Queens) na Fatuma Bashiri (Simba Queens).
Wengine ni Fatuma Gotagota (Mburahati Queens), Fatuma Khatib
(Mburahati Queens), Fatuma Mustafa (Sayari), Fatuma Omari (Sayari), Hanifa Idd
(Uzuri Queens), Maimuna Said (JKT), Mwajuma Abdallah (JKT), Mwanahamisi Omari (Mburahati Queens) na
Mwanaidi Khamis (Uzuri Queens).
Mwapewa Mtumwa (Temeke), Rukia Khamis (Sayari), Semeni Abeid
(Tanzanite), Siajabu Hassan (Evergreen), Tatu Salum (Makongo Sekondari), Upendo
Jeremiah (Pangani, Tanga), Veneranda Mbano (Tanzanite), Zena Khamis (Mburahati
Queens) na Zena Said (Uzuri Queens).



.png)
0 comments:
Post a Comment