TIMU ya taifa ya wanawake, Twiga Stars imeingia Nusu Fainali ya Kombe la COSAFA baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Botswana kwenye mchezo wa Kundi B leo Uwanja wa Nelson Mandela Bay Jijini Port Elizabeth, Afrika Kusini.
Mabao ya Tanzania leo yamefungwa na Deonisia Minja dakika ya sita na Mwanahamisi Omary dakika ya 79 na kwa matokeo hayo Twiga Stars inafikisha pointi sita kufuatia kuichapa na Zimbabwe 3-0 kwenye mechi ya kwanza Jumatano.
0 comments:
Post a Comment