NAHODHA Mbwana Ally Samatta jana amejiunga na kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania kuelekea mchezo wa pili wa Kundi J kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Madagascar Jumanne Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Samatta alikosekana kwenye mchezo wa kwanza Alhamisi Taifa Stars ikilazimisha sare ya 1-1 na wenyeji, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Uwanja wa TP Mazembe Jijini Lubumbashi.
Kilichomkwamisha Samatta ni kushughulikia ubamisho wake wa mkopo kutoka Fenerbahce ya Uturuki kwendaRoyal Antwerp ya Ubelgiji.
0 comments:
Post a Comment