• HABARI MPYA

    Friday, January 25, 2019

    RAMOS AFUNGA MAWILI REAL MADRID YASHINDA 4-2 KOMBE LA MFALME

    Nahodha wa Real Madrid, Sergio Ramos akishangilia baada ya kuifungia timu yake mabao mawili, dakika za 42 kwa penalti na 77 katika ushindi wa 4-2 dhidi ya Girona kwenye mchezo wa kwanza wa Robo Fainali ya Kombe la Mfalme jana Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid. Mabao mengine ya Real Madrid yalifungwa na Lucas Vázquez dakika ya 18 na Karim Benzema dakika ya 80, wakati ya Girona yalifungwa na Anthony Lozano dakika ya saba na Alex Granell kwa penalti dakika ya  66 na timu hizo zitarudiana Januari 31 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RAMOS AFUNGA MAWILI REAL MADRID YASHINDA 4-2 KOMBE LA MFALME Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top