• HABARI MPYA

    Saturday, January 19, 2019

    LIVERPOOL YAENDELEA KUNG'ARA ENGLAND, YAICHAPA PALACE 4-3

    Sadio Mane akiifungia bao la ushindi Liverpool dakika ya 90 na ushei ikiilaza Crystal Palace 4-3 usiku wa leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Anfield. Mabao mengine ya Liverpool yamefungwa na Mohamed Salah mawili, dakika ya 46 na 75 na Roberto Firmino dakika ya 53, wakati ya Crystal Palace yamefungwa na Andros Townsend dakika ya 34, James Tomkins dakika ya 65 na Max Meyer dakika ya 90 na ushei.
    Ushindi huo unaifanya Liverpool ifikishe pointi 60 baada ya kucheza mechi 23, ikiendelea kuongoza Ligi Kuu England kwa pointi saba zaidi ya mabingwa watetezi, Manchester City wanaofuatia katika nafasi ya pili 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YAENDELEA KUNG'ARA ENGLAND, YAICHAPA PALACE 4-3 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top