• HABARI MPYA

    Monday, January 21, 2019

    MESSI AFUNGA BAO LA 25 MECHI YA 24 BARCA IKISHINDA 3-1

    Lionel Messi akishangilia baada ya kuifungia Barcelona bao la tatu dakika ya 90 na ushei katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Leganes kwenye mchezo wa La Liga usiku wa jana Uwanja wa Camp Nou, hilo likiwa bao la 25 kwa Muargentina huyo katika mechi 24 za mashindano yote msimu huu. Mabao mengine ya Barca yamefungwa na Ousmane Dembele dakika ya 32 na Luis Suarez dakika ya 71 na kwa ushindi huo, timu hiyo ya Katalunya inafikisha pointi 46 baada ya kucheza mechi 20 ikiendelea kuongoza La Liga kwa pointi tano zaidi ya Atlético Madrid wanaofuatia nafasi ya pili na 10 zaidi ya Real Madrid walio nafasi ya tatu 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AFUNGA BAO LA 25 MECHI YA 24 BARCA IKISHINDA 3-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top