• HABARI MPYA

    Saturday, January 26, 2019

    MAN UNITED YAIGONGA ARSENAL 3-1 EMIRATES NA KUSONGA MBELE FA

    Wachezaji wa Manchester United wakimpongeza mwenzao, Alexis Sanchez baada ya kufunga bao la kwanza dakika ya 31 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya timu yake ya zamani, Arsenal kwenye mchezo wa Raundi ya Nne Kombe la FA England usiku wa jana Uwanja wa Emirates, London. Mabao mengine ya Man United yalifungwa na Jesse Lingard dakika ya 33 na Anthony Martial dakika ya 82, wakati la Arsenal limefungwa na Pierre-Emerick Aubameyang dakika ya 43.
    Kwa ushindi huo wa mwendelezo mzuri wa kocha mpya wa muda, ole Gunnar Solskjaer Mashetani Wekundu wanakwenda Raundi ya Tano ya Kombe la FA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YAIGONGA ARSENAL 3-1 EMIRATES NA KUSONGA MBELE FA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top