Beki Mbrazil, David Luiz akishangilia baada ya kufunga penalti ya nne ya Chelsea kuipeleka Fainali ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Carabao Cup kufuatia ushindi wa penalti 4-2 dhidi ya Tottenham Hotspur jana Uwanja wa Stamford Bridge mjini London katika mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali. Chelsea ilishinda 2-1 na kufanya sare ya jumla ya 2-2 kufuatia kufungwa 1-0 kwenye mchezo wa kwanza na mbali ya Luiz wengine waliofunga penalti za The Blues ni Willian, Azpilicueta na Jorginho, wakati Christian Eriksen na Erik Lamela pekee walifunga za Spurs, huku Eric Dier na Lucas Moura wakikosa. Chelsea itakutana na Manchester City katika fainali Februari 24 Uwanja wa Wembley mjini London PICHA ZAIDI GONGA HAPA
U20 Women's World Cup: African Origin Travels and Sports Tourism appointed Ghana's official travel and hospitality agency
-
African Origin Travels and Sports Tourism have been appointed Ghana's
official Travel and Hospitality Agency for the 2022 FIFA U20 Women's World
Cup to be ...
Dakika 33 zilizopita
0 maoni:
Chapisha Maoni