• HABARI MPYA

    Sunday, August 30, 2015

    MAN UNITED YAFUMULIWA 2-1 UGENINI NA SWANSEA, BAFETIMBI NA ANDRE AYEW HAO

    MANCHESTER United imepoteza mechi ya ugenini mbele ya Swansea City baada ya kufungwa mabao 2-1 katika Ligi Kuu ya England jioni ya leo.
    Juan Mata alianza kuifungia Man United dakika ya 48, kabla ya Andre Ayew kuisawazishia Swansea dakika ya 61 na Befetimbi Gomis kufunga la ushindi dakika tano baadaye.
    Kikosi cha Swansea kilikuwa; Fabianski, Naughton, Fernandez, Williams, Taylor, Cork, Shelvey/Bartley dk88, Ayew, Sigurdsson, Routledge/Ki dk58 na Gomis/Eder dk80.
    Manchester United; Romero, Darmian, Smalling, Blind, Shaw, Schneiderlin/Carrick dk70, Schweinsteiger, Mata/Young dk70, Herrera/Fellaini dk76, Depay na Rooney.
    Bafetimbi Gomis akishangilia kwa staili yake maarufu baada ya kuifungia Swansea bao la ushindi leo PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YAFUMULIWA 2-1 UGENINI NA SWANSEA, BAFETIMBI NA ANDRE AYEW HAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top