• HABARI MPYA

    Saturday, August 22, 2015

    BAO LA ROONEY LAKATALIWA, MAN UNITED YATOA SARE 0-0 NA NEWCASTLE

    TIMU ya Manchester United imepunguzwa kasi katika Ligi Kuu ya England baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Newcastle United Uwanja wa Old Trafford mchana wa leo.
    Nahodha wa Manchester United, Wayne Rooney alimtungua kipa Tim Krul kuifungia timu yake kipindi cha kwanza, lakini akanyooshewa kibendera cha kuotea.
    Kikosi cha Manchester United kilikuwa; Romero, Darmian/Valencia dk77, Smalling, Blind, Shaw, Schneiderlin, Schweinsteiger/Carrick dk59, Mata, Januzaj/Hernandez dk67, Depay na Rooney.
    Newcastle United: Krul, Coloccini, Mbemba, Taylor, Haidara, Anita, Colback, Obertan/Thauvin dk69, Wijnaldum, Perez/Tiote dk78 na Mitrovic/Cisse dk88.
    Beki wa Newcastle, Steven Taylor akinyoosha mkono juu kupinga bao la Wayne Rooney ambalo lilikataliwa leo Old Trafford kwa sababu alikuwa ameotea PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BAO LA ROONEY LAKATALIWA, MAN UNITED YATOA SARE 0-0 NA NEWCASTLE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top