• HABARI MPYA

    Tuesday, August 25, 2015

    BALOTELLI AREJEA RASMI AC MILAN BAADA YA KUCHEMSHA LIVERPOOL

    Mario Balotelli amerejea AC Milan kwa mkopo leo baada ya kufuzu vipimo vya afya PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    BALOTELLI NA LIGI ALIZOCHEZA 

    Liverpool (2014-15): Mechi 16 bao moja
    AC Milan (2013-14): Mechi 43 mabao 26
    Man City (2010-13):  Mechi 54 mabao 20
    Inter Milan (2006-10): mechi tano mabao mawili
    Jumla ya gharama zake: Pauni Milioni 59 
    MSHAMBULIAJI Mario Balotelli amerejea kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu AC Milan ya Italia baada ya kushindwa kung'ara Liverpool ya England.
    Mshambuliaji huyo ambaye amekuwa akifanya mazoezi nje ya kikosi cha kwanza Liverpool kwa karibu mwezi wote, alikuwa mjini Milan tangu mwishoni mwa wiki kushughulikia mpango wa kuondoka Anfield.
    Balotelli alipigwa picha akitoka kwenye gari aina ya Audi nyeusi akiwa amevalia Puma nyekundu akiingia katika hospitali kwa vipimo kabla ya kusaini Mkataba. Taarifa ya Milan imesema: "Saa 2:26 asubuhi hii, Mario Balotelli amewasili zahanati ya La Madonnina kufanyiwa vipimo vya afya,".
    Balotelli, aliyekuwa analipwa Pauni 80,000 kwa wiki Liverpool, alifunga bao moja tu Ligi Kuu ya England katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Tottenham Februari - na mengine matatu katika mashindano ya vikombe. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BALOTELLI AREJEA RASMI AC MILAN BAADA YA KUCHEMSHA LIVERPOOL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top