• HABARI MPYA

    Saturday, December 13, 2014

    MAYWEATHER ATHIBITISHA; "NITAZIPIGA NA PACQUIAO MEI 2, 2005"

    HATIMAYE bondia Floyd Mayweather Jnr ametaja Mei 2 mwakani kuwa tare he ya pambano lake na Manny Pacquiao.
    Tetesi juu ya ujio wa poambano hilo la utajiri mkubwa zimezidi kuenea tangu Pacman aonyeshe kiwango kizuri wakati anampiga Chris Algieri mjini Macau, China wiki mbili zilizopita.
    Sasa Mayweather, anazipa kazi ya ziada moja ya kampuni zake promosheni ya matukio kwa kusema: "Nitapigana na Pacquiao? Sahihi,". 
    Floyd Mayweather's has confirmed that he will fight with Manny Pacquiao in 2015
    Floyd Mayweather amethibitisha pambano lake na Manny Pacquiao litafanyika mwaka 2015
    Pacquiao (right) called out Mayweather to fight him after beating Chris Algieri in November
    Pacquiao (kulia) alimtaka Mayweather wapambane baada ya kumpiga Chris Algieri mwezi Novemba

    Alipoulizwa litakuwa pambano lake lijalo, akajibu; "Sahihi," na alipotakiwa kutaja tarehe ya pambano lake lijalo, akasema; "Mei 2, sahihi,".
    Bondia huyo ambaye hajapoteza pambano na anayesifiwa kwamba ndiye mkali wa kurupa makonde duniani ameongeza; "Watu wanalitaka hikli pambano. Nalitaka. Kikwazo pekee kilikuwa Bob Arum (promota wa Pacquiao) lakini nafikiri mabondia wote wanalitaka. Hivyo ni wakati wa kupambana,"amesema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAYWEATHER ATHIBITISHA; "NITAZIPIGA NA PACQUIAO MEI 2, 2005" Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top