• HABARI MPYA

    Tuesday, March 20, 2012

    MESSI BADO BAO MOJA TU

    Messi
    MWANASOKA bora wa dunia, Lionel Messi anahitaji bao moja tu kufikia rekodi ya ufungaji mabao ya klabu yake, Barcelona baada ya rekodi ya Cesar Rodriguez kurekebisha na kupunguziwa mabao hadi kuwa 232 kutoka 235, imesema klabu hiyo ya La Liga.
    Idara ya Takwimu wa Barca kwa pamoja na gazeti la La Vanguardia imepitia kwa makini idadi ya mabao ya Rodriguez miaka ya 1950 na kutoa masahihisho hayo.
    Takwimu mpya zinaonyesha aliongezewa mabao matatu katika mabao aliyofunga, ilisema Barca katika taarifa iliyoitoa kwe nye tovuti yake (www.fcbarcelona.com).
    Messi, ambaye amefunga mabao 51 kwenye mashindano yote msimu huu, anaweza kuvun ja rekodi hiyo wakati Barca ikiwa mwenyeji wa Granada katika La Liga baadaye leo.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, huu ni msimu wake wa nane Barca.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI BADO BAO MOJA TU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top