• HABARI MPYA

    Friday, June 23, 2023

    YANGA YAPIGWA NA DODOMA JIJI, SIMBA YADROO, AZAM YASHINDA


    VIGOGO, Simba na Yanga wameanza kwa kusuasua Ligi ya Vijana chini ya umri wa miaka 20 katika mechi zao za leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
    Wakati Simba imelazimishwa sare ya bila kufungana na Kagera Sugar katika mchezo wa Kundi D, Yanga imechapwa 1-0 na Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Kundi B.
    Mechi nyingine za leo, Azam FC imeibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Ihefu katika mchezo wa Kundi D, wakati Tanzania Prisons imeitandika Polisi Tanzania 4-2 katika mchezo wa Kundi B mechi zote zikichezwa hapo hapo Chamazi Alhamisi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA YAPIGWA NA DODOMA JIJI, SIMBA YADROO, AZAM YASHINDA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top