• HABARI MPYA

    Wednesday, June 07, 2023

    SHEREHE ZA UBINGWA YANGA JUMAMOSI DAR ITAZIZIMA


    SHEREHE za ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara za Yanga zitafanyika Jumamosi kuanzia 3:00 asubuhi timu itakapokuwa inarejea kutoka Mbeya baada ya mchezo wake wa mwisho wa ligi hiyo dhidi ya Tanzania Prisons Uwanja wa Sokoine.
    Kikosi kitaondoka Mbeya mapema tu asubuhi baada ya mchezo wake na Prisons na kulakiwa na maelfu ya mashabiki wake huku wachezaji wakipanda kwenye gari maalum la kuonyesha Kombe lao.
    Huu ni ubingwa wa pili mfululizo kwa Yanga na wa 29 jumla ambao unawafanya watanue rekodi yao ya kutwaa mara nyingi zaidi hadi mara saba zaidi ya watani, Simba.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SHEREHE ZA UBINGWA YANGA JUMAMOSI DAR ITAZIZIMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top