Mabao ya Mashujaa yamefungwa na Abihud Mtumbuka dakika ya 24, Asanga Stallone dakika ya 69 na Shadrack Ntabindi kwa penalti dakika ya 78, wakati la Mbeya City alijifunga Aziz Sibo dakika ya 63.
Timu hizo zitarudiana Alhamisi Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya na Mbeya City itatakiwa kushinda 2-0 ili kufuzu kwa sheria ya mabao ya ugenini.
Mshindi wa jumla atapanda Ligi Kuu na timu itakayofungwa itakwenda kucheza Ligi ya Championship. Ikumbukwe Mashujaa inacheza mchujo huu ikitoka Championship na Mbeya City imetoka Ligi Kuu.
0 comments:
Post a Comment