• HABARI MPYA

    Wednesday, December 01, 2021

    TANZANIA YAFUZU KOMBE LA DUNIA SOKA WALEMAVU


    TIMU ya taifa ya Tanzania 'Tembo Warriors' imetinga Nusu Fainali ya Michuano ya Soka kwa Walemavu Afrika (CANAF 2021)
    baada ya ushindi wa 5-0 dhidi ya Cameroon Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
    Mabao ya Tembo yamefungwa na Hallfan Kyanga mawili dakika ya  pilu na 15 , Ramadhan Chomole  dakika ya 18, na Frank Ngailo mawili pia, dakika ya 36 na 44.
    Kwa matokeo hayo, Tembo imekuwa  timu ya kwanza kufuzu Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Uturuki. 
    Katika mechi zote za mashindano haya Tanzania imepoteza mechi moja tu dhidi ya Uganda mbayo ilifungwa 1-0, lakini mechi nyingine imezichapa Morocco 2-1 na Sierra Leone 1-0.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA YAFUZU KOMBE LA DUNIA SOKA WALEMAVU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top