MABINGWA wa Tanzania, SIMBA SC wameachana na kocha wao, Mnyarwanda Thierry Hitimana baada ya miezi mitatu tu kazini.
Hitimana alitambulishwa kama kocha Msaidizi Simba Septemba 11 na baada ya Mfaransa, Didier Gomes Da Rosa kujiuzulu Oktoba 26, Mnyarwanda huyo akakaimu nafasi ya Kocha Mkuu.
Lakini kufuatia kuletwa kocha mpya, Mspaniola Pablo Franco Martin Novemba 10, Hitimana anaonyeshwa mlango wa kutokea Msimbazi.
0 comments:
Post a Comment