WENYEJI, Mtibwa Sugar wamelazimishwa sare ya bila mabao na KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Manungu Complex, Turiani mkoani Morogoro.
Kwa sare hiyo, Mtibwa Sugar inafikisha pointi sita na inaendelea kuzibeba timu nyingine zote 15, wakati KMC imetimiza pointi 10 na kusogea nafasi ya tisa baada ya wote kucheza mechi tisa sasa.
0 comments:
Post a Comment