MABINGWA watetezi, Simba SC wamefanikiwa kwenda Raundi ya Nne ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Tanzania usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee mshambuliaji Mtanzania mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Kibu Dennis Prosper dakika ya 27.
0 comments:
Post a Comment