MCHEZO wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baina ya wenyeji, Kagera Sugar na mabingwa watetezi, Simba SC uliopangwa kufanyika Saa 10:00 jioni ya leo Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba umeahirishwa hadi hapo utakapopngiwa tarehe nyingine.
Taarifa ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imesema kwamba sababu za kuuahirisha mchezo huo ni wachezaji 16 kati ya 22 waliosafiri na Simba Bukoba wamegundulika kuwa na homa ya mafua.
0 comments:
Post a Comment