MABINGWA watetezi, Simba Queens wameendelea kugawa maumivu kwa wapinzani katika Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara baada ya kuichapa Oysterbay Girls 8-0 jioni ya leo Uwanja wa Mo SIMBA Arena, Bunju, Dar es Salaam.
Mabao ya Simba Queens yamefungwa na Aisha Djafar matatu, Opa Clement na Aisha Mnunka kila mmoja mawili, wakati la nane Oysterbay Girls walijifunga.
0 comments:
Post a Comment