• HABARI MPYA

    Wednesday, September 08, 2021

    ABDI BANDA AJIUNGA NA MTIBWA SUGAR

     MABINGWA wa zamani wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Mtibwa Sugar wamemsajili beki wa kati, Abdi Hassan Banda kutoka TS Galaxy ya Afrika Kusini.
    Banda aliyezaliwa Mei 20 mwaka 1995, aliibukia Coastal Union ya Tanga mwaka 2012 hadi 2014 alipohamia Simba SC ya Dar es Salaam .
    Alicheza Simba SC hadi mwaka 2017 alipokwnda Afrika Kusini ambako alicheza Baroka FC hadi 2019 alipohamia Highlands Park kabla ya kutua TS Galaxy msimu uliopita.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ABDI BANDA AJIUNGA NA MTIBWA SUGAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top