Nyota wa zamani wa AC Milan, George Weah anasubiri matokeo ya uchaguzi wa Urais Liberia kuwania kumrithi Ellen Johnson Sirleaf
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amedanganyika na habari feki zinazoenezwa kwamba George Weah ameshinda Urais wa Liberia.
Wenger, ambaye alimgundisha mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 51 katika klabu ya Monaco kuanzia mwaka 1988 hadi 1992, ametumia tovuti ta The Gunners kumpongeza Weah. Kwa bahati mbaya, Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 67, matokeo halisi hayajatangazwa.
Wenger amesema, “Ningependa kumpongeza mmoja wa wachezaji wangu wa zamani, ambaye amekuwa Rais wa Liberia, George Weah.
Weah, Mwanasoka Bora wa zamani wa Mwaka wa FIFA, anawania tena Urais wa Liberia katika uchaguzi uliofanyika Jumanne baada ya kushindwa katika chaguzi mbili za awali.
Arsene Wenger (kulia) akiwa na George Weah wakati wanafanya naye jazi Monaco kati ya mwaka 1988 na 1992
Weah anabaki kuwa Mwanasoka pekee Mwafrika aliyeshinda tuzo yaBallon d'Or mwaka 1995.
Ni Wenger alimvuta Weah Ulaya mwaka 1988 alipomnunua Monaco akitokea Tonnerre Yaounde ya Cameroon. Kabla ya hapo alicheza Mighty Barrolle, Invincible Eleven za kwao Liberia na Africa Sports ya Ivory Coast.
Alijiunga na Paris Saint-German ya Ufaransa mwaka 1992, ambako alicheza kwa misimu mitatu kabla ya kuhamia AC Milan ya Italia.
Amecheza pia Chelsea kwa mkopo, Manchester City zote za England, Marseille ya Ufaransa na Al-Jazira ya Saudi Arabia.
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amedanganyika na habari feki zinazoenezwa kwamba George Weah ameshinda Urais wa Liberia.
Wenger, ambaye alimgundisha mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 51 katika klabu ya Monaco kuanzia mwaka 1988 hadi 1992, ametumia tovuti ta The Gunners kumpongeza Weah. Kwa bahati mbaya, Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 67, matokeo halisi hayajatangazwa.
Wenger amesema, “Ningependa kumpongeza mmoja wa wachezaji wangu wa zamani, ambaye amekuwa Rais wa Liberia, George Weah.
Weah, Mwanasoka Bora wa zamani wa Mwaka wa FIFA, anawania tena Urais wa Liberia katika uchaguzi uliofanyika Jumanne baada ya kushindwa katika chaguzi mbili za awali.
Arsene Wenger (kulia) akiwa na George Weah wakati wanafanya naye jazi Monaco kati ya mwaka 1988 na 1992
Weah anabaki kuwa Mwanasoka pekee Mwafrika aliyeshinda tuzo yaBallon d'Or mwaka 1995.
Ni Wenger alimvuta Weah Ulaya mwaka 1988 alipomnunua Monaco akitokea Tonnerre Yaounde ya Cameroon. Kabla ya hapo alicheza Mighty Barrolle, Invincible Eleven za kwao Liberia na Africa Sports ya Ivory Coast.
Alijiunga na Paris Saint-German ya Ufaransa mwaka 1992, ambako alicheza kwa misimu mitatu kabla ya kuhamia AC Milan ya Italia.
Amecheza pia Chelsea kwa mkopo, Manchester City zote za England, Marseille ya Ufaransa na Al-Jazira ya Saudi Arabia.
0 comments:
Post a Comment