KIUNGO wa Manchester City, Yaya Toure ametemwa kwenye kikosi cha Ivory Coast kitakachomenyana na Gambia katika mchezo wa kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika mwishoni mwa wiki kwa sababu ya majeruhi.
Taarifa ya Shirikisho la Soka Ivory Coast imesema jana kwamba Nahodha huyo wa Tembo hatakuwamo kwenye kikosi hicho kwa sababu ya majeruhi.
Taarifa ya Shirikisho la Soka Ivory Coast imesema jana kwamba Nahodha huyo wa Tembo hatakuwamo kwenye kikosi hicho kwa sababu ya majeruhi.
Toure alionekana kumaliza msimu wa Ligi Kuu ya England akiwa na klabu yake, Manchester City mwezi uliopita bila tatizo lolote.
Pamoja na hayo, shirikisho la soka la nchi hiyo limesema ni majeruhi bila kutoa taarifa zaidi.
Kiungo Yaya Toure ameenguliwa kwenye kikosi cha Ivory Coast kitachomenyana na Gambia mwishoni mwa wiki kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika
Kocha wa muda wa Tembo, Ibrahima Kamara pia atamkosa kaka yake Yaya, Kolo Toure, ambaye amestaafu soka ya kimataifa baada ya kuiwezesha Ivory Coast kutwaa Kombe la AFCON nchini Equatorial Guinea mwanzoni mwa mwaka huu.
Kikosi cha Tembo kitasafiri hadi Libreville kikiwa na nyota wengine akiwemo mchezaji mwenzake Yaya pale Man City, Wilfried Bony, Gervinho na Salomon Kalou, ambao walikuwemo kwenye timu iliyobeba Kombe la Mataifa ya Afrika Februari.
Mchezo wa Jumapili mjini Libreville ni sehemu ya mechi za ufunguzi za mbio za AFCON mwaka 2017 nchini Gabon.
Salomon Kalou, Wilfried Bony na Gervinho wote watakuwemo kwenye kikosi cha Ivory Coast


.png)
0 comments:
Post a Comment