• HABARI MPYA

    Thursday, June 25, 2015

    TANZANITE YAINGIA KAMBINI

    Na Baraka Kizguto, DAR ES SALAAM
    TIMU ya taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanawake wenye umri chini ya miaka 20 (U-20) Tanzanite Stars, imeingia kambini jana jioni Mbande jijini Dar es salaam na itakua ikifanya mazoezi katika uwanja wa Azam Complex.
    Kikosi cha wacheaji 22 chini ya Kocha Mkuu Rogasian Kaijage kinafanya mazoezi asubuhi na jioni katika uwnaja wa Azam uliopo Chamazi kujiandaa na mchezo dhidi ya U-20 ya Zambia utakaofanyika kati ya tarehe 10, 11 na 12 July jijini Dar es salaam.
    Mchezo huo dhidi ya Zambia ni wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Wanawake za Dunia wenye umri chini ya miaka ya 20, zitakazofanyika nchini Papua New Guinea mwaka 2016.

    Wachezaji waliopo kambini ni, Najiati Abbasi, Zuwena Aziz, Shelder Boniface, Stumai Abdallah, Donisia Daniel, Tatu Iddy (Evergreen Queens), Niwael  Khalfani, Maimuna Hamis (Mburahati Queens), Anastazia Anthony, Amisa Athumani, Amina Ramadhani, Neem Paulo (JKT Queens).
    Wengine ni Asha Shaban, Rebeka Daniel, Brandina Wincelaus (Tanga), Happines Hezroni, Jane Cloudy (JKT Queens), Wema Richard, Gerwa Lugomba, Sadda Ramadhani (Uzuri Queens), Anna Hebron (Evergreen Queens) na Shehati Mohamed (Mburahati Queens)
    Aidha wachezaji Monica Henry, Tumaini Michael (Uzuri Queens), Diana Msewa (Mbeya), na Vailet Nicolaus (Evergreen) bado hawajaripoti kambini wanaombwa kuripoti  na kuungana na wenzao katika maandalizi ya mchezo huo dhidi ya Zambia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANITE YAINGIA KAMBINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top