• HABARI MPYA

    Tuesday, June 30, 2015

    TAIFA STARS YA BAADAYE KWENDA 'KUPASHA' MADAGASCAR

    Na Baraka Kizuguto, DAR ES SALAAM
    KIKOSI cha timu ya Taifa cha vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U-15) leo kinarejea jijini Dar es salaam kikitokea mkoani Mbeya ambapo jana kiliibuka na ushindi wa ushindi wa mabao 4-1.
    U15 ambayo inaandaliwa kwa ajili ya kuwania kufuzu kwa fainali za vijana chini ya miaka 17 barani Afrika kilikua na ziara ya michezo ya kirafiki miwili jijini Mbeya ambapo katika mchezo wa awali pia kiliibuka na ushindi wa mabao 3-0.
    Mara baada ya kurejea leo jioni jijini Dar es salaam, kambi ya timu hiyo itavunjwa mpaka watakapokutana tena mwisho wa mwezi ujao kwa ajili ya kuelekea visiwani zanzibar kwa jili ya michezo ya kirafiki.

    Lengo la michezo hiyo ya kirafiki ni kutoa nafasi ya kocha Bakari Shime kutambua uwezo wa vijana wake na kuongeza wachezaji wengine katika kikosi hicho kisha kuandaa kikosi bora kitakachoshirki kuwania kufuzu kwa fainali hizo zitakazofanyika nchini Madagascar mwaka 2017.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS YA BAADAYE KWENDA 'KUPASHA' MADAGASCAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top