• HABARI MPYA

    Saturday, November 15, 2014

    XAVI ASEMA KWA UKABAJI WA MABEKI WA ENGLAND, MESSI AKIHAMIA LIGI KUU ATAKUWA TISHIO KULIKO LA LIGA

    KIUNGO wa Barcelona, Xavi anaamini mchezaji mwenzake nyota, Lionel Messi anaweza kuwa 'babu kubwa' hata kwenye Ligi Kuu ya England kuliko alivyo sasa kwenye La Liga.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 34, ambaye ameshinda mataji saba ya La Liga na matatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati wake katika klabu hiyo, anaamini falsafa ya ulinzi ya England itampa fursa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kutamba.
    Ameiambia BBC Michezo: "Nafikiri atakuwa mzuri hata kwenye Ligi Kuu (England) kwa sababu haina ulinzi mkali,". 
    Lionel Messi has established himself as one of, if not the best player in the world at Barcelona
    Lionel Messi amejipambanua kama mchezaji wa kipekee duniani akiwa Barcelona

    "Wakati wanapojilinda dhidi ya Barcelona, wao [Klabu za England] wanacheza mfumo wa mmoja dhidi ya mmoja, wanakaba kwa kujituma na kutumia nguvu nyingi. Lakini Leo anaweza kupata nafasi nyingi kuliko La Liga,".
    Licha ya maelezo hayo ya Xavi, inaonekana kama Messi hana mango kabisa wa kuhamia Ligi Kuu ya England, katakana na kurudia kusema anafurahia kubaki Barcelona kumalizia soka yake huko.  
    Messi scored his first goal on English soil at Wembley in the 2011 Champions League final against Man United
    Messi alifunga bao lake la kwanza kwenye ardhi ya England Uwanja wa Wembley mwaka 2011 katika fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Man United
    Xavi and Messi line up a free-kick for the Catalan giants during their La Liga clash with Rayo Vallecano
    Xavi ana Messi wakijadiliana kabla ya kupiga mpira wa adhabu katika mechi ya La Liga dhidi ya Rayo Vallecano

    Kwa msimu huu, mshambuliaji huyo wa Argentina tayari amefunga mabao 11 katika mechi 15 za vigogo hao wa Katalunya, wakiwa wanazidiwa pointi mbili na wapinzani wao, Real Madrid waliopo kileleni mwa La Liga.
    Messi pia anakaribia kuvunja rekodi nyingine baadaye mwezi huu, kwa kumpiku Raul kwa ufungaji wa mabao mengi zaidi katika katika Ligi ya Mabingwa (mabao 71), baada ya kufinikiwa kumfikia kutokana na kufunga katika ushindi wa  2-0 dhidi ya Ajax mapema mwezi huu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: XAVI ASEMA KWA UKABAJI WA MABEKI WA ENGLAND, MESSI AKIHAMIA LIGI KUU ATAKUWA TISHIO KULIKO LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top