• HABARI MPYA

    Saturday, November 15, 2014

    ROONEY ATUPIA MOJA MECHI YA 100, WELBECK MBILI ENGLAND IKIICHAPA 3-1 SLOVENIA KUFUZU EURO

    TIMU ya taifa ya England imeichapa Slovenia mabao 3-1 katika mchezo wa Kundi D kufuzu Euro 2016 Uwanja wa Wembley, Nahodha Wayne Rooney akizawadiwa 'kofia ya dhahabu' baada ya kuwa mchezaji mdogo aliyetimiza mechi 100 kihistoria England.
    Nahodha wa Slovenia, Bostjan Cesar alikuwa mwenye bahati kwa kutopewa kadi nyekundu baada ya kumpiga usoni Adam Lallana katika mchezo ambao, England walifungwa bao la kwanza katika kampeni hizo za kufuzu, baada ya Jordan Henderson kujifunga kipindi cha pili.
    Nahodha Rooney aliisawazishia kwa penalti baada ya yeye mwenyewe kuchezewa rafu akifunga bao lake la 44 timu ya taifa.
    Mshambuliaji wa Arsenal, Danny Welbeck akafunga mabao mawili ndani ya dakika sita kuihakikishia England ushindi huo na rekodi safi.
    Kikosi cha England kilikuwa; Hart, Clyne, Cahill, Jagielka, Gibbs, Henderson, Wilshere, Lallana/Milner dk6, Welbeck, Rooney na Sterling/Oxlade-Chamberlain. 
    Slovenia: Handanovic, Brecko, Ilic, Cesar, Sturna, Mertelj, Kurtic/Rotman dk75, Birsa/Lazarevic dk63, Kampl, Kirm/Ljubijankic dk78 na Novakovic.
    Rooney clasps his hands together towards the sky after scoring from the penalty spot
    Wayne Rooney akipunga mkono angani baada ya kufunga kwa penalti
    Welbeck's shot hits the ground before beating the keeper to give England the lead for the first time
    Danny Welbeck akiifungia England leo

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2836035/England-3-1-Slovenia-Wayne-Rooney-marks-century-equaliser-Danny-Welbeck-double-sees-Three-Lions-roar-finals.html#ixzz3JAbzrQ4w 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ROONEY ATUPIA MOJA MECHI YA 100, WELBECK MBILI ENGLAND IKIICHAPA 3-1 SLOVENIA KUFUZU EURO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top