• HABARI MPYA

    Saturday, November 15, 2014

    ADVOCAAT ABWAGA MANYANGA SERBIA BAADA YA KICHAPO CHA 3-1 KUTOKA DENMARK JANA

    Advocaat amebwaga manyanga Serbia
    MHOLANZI Dick Advocaat amejiuzulu ukocha wa Serbia baada ya kipigo cha mabao 3-1 nyumbani kutoka kwa Denmark katika mechi ya kufuzu Euro 2016, Shirikisho la Soka Serbia (FSS) limesema leo.
    "FSS inamshukuru Advocaat kwa kuonyesha uadilifu wa kitaaluma na tunasikitika ushirikiano wetu na yeye umeisha vibaya," imesema bodi hiyo ya soka.
    "Tunamtakia kila la heri huko katika mustakabali wake baadaye wa kazi,". kwa upande wake, Advocaat amesema: "Presha ambayo ilikuwa kila mahala ilikuwa ni kubwa kuimudu katika timu hii na sijawahi kukutana na wakati mgumu kama huu katika maisha yangu ya kazi,".
    "Serbia inatakiwa haraka kwenda kutafuta njia nzuri na ninaishukuru FSS kwa sapoti yao,". Kipigo cha Denmark, katika mechi iliyochezwa bila mashabiki inaiweka shakani nafasi ya Serbia kufuzu kutokana na kuambulia pointi moja katika mechi mbili.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ADVOCAAT ABWAGA MANYANGA SERBIA BAADA YA KICHAPO CHA 3-1 KUTOKA DENMARK JANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top