BONDIA Wladimir Klitschko amefanikiwa kutetea kwa mara ya 17 mfululizo taji lake, baada ya kumpiga Knockout Kubrat Pulev Raundi ya tano mjini Hamburg jana usiku.
Bingwa huyo wa uzito wa juu wa IBF, WBA na WBO alimbwaga chini mara mbili mpinzani wake katika raundi ya kwanza na ikaonekana kama pambano hilo halitafika mbali.
Pulev aliangushwa chini tena katika raundi ya tatu, lakini tena akafanikiwa kuinuka kabla ya kukutana na ngumi ya mkono wa kushoto ya Klitschko raundi ya tano na kumfanya Mbulgaria huyo apoteze pambano la kwanza baada ya kupanda ulingoni mara 21 na Klitschko kuendeleza rekodi yake ya kushinda mapambano 63 na kupoteza matatu, 53 kati ya hayo kwa Knockout.
Mbabe wa Ukraine ametetea taji lake la IBF uzito wa juu kwa ushindi wa raundi ya tano nchini Ujerumani
Klitschko akimkalisha Mbulgaria mjini Hamburg
PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/boxing/article-2836209/Wladimir-Klitschko-retains-IBF-heavyweight-title-devastating-fifth-round-knockout-Bulgarian-Kubrat-Pulev-Hamburg.html#ixzz3JDGWJLun
0 comments:
Post a Comment