MTOTO mkubwa wa Zinedine Zidane, Enzo jana amecheza mechi yake ya kwanza katika kikosi cha Real Madrid B kikishinda 2-1 nyumbani dhidi ya Conquense Jumapili- huku baba yake akiwa benchi la Ufundi.
Kocha Msaidizi wa Real Castilla, Zinedine Zidane alimuingiza mwanawe huyo zikiwa zimesali dakika mbili, lakini akatumia muda huo mfupi kuonyesha vitu vyake.
Kinda huyo wa umri wa miaka 19 alikaribia kufunga baada ya kufumua shut zuri, kiasi cha kujiwekea mazingira mazuri ya kupata namba kwenye kikosi cha kwanza kinachocheza Ligi ya Segunda B, ambayo ni Daraja la Tatu nchini Hispania.
Enzo Zidane (kulia, pichani ya Machi), mtoto wa Zinedine, jana amecheza mechi yake ya kwanza Real Madrid Castilla
Zinedine Zidane ni kocha Msaidizi wa timu ya vijana ya Real Madrid, inayojulikana kama Castilla na jana alimuingiza mwanawe kucheza akitokea benchi
Zinedine Zidane (kushoto), akiichezea Real Madrid mwaka 2006, na kijana wake Enzo, akiichezea timu ya vijana ya klabu hiyo Machi


.png)
0 comments:
Post a Comment