KLABU ya Manchester City imetangaza kumuuza Javi Garcia klabu ya Zenit St Petersburg.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 amefuzu vipimo vya afya na kuafiki vipengele vya Mkataba binfasi leo, kuhamia klabu hiyo ya Urusi kwa dau la Pauni Milioni 13.
Garcia hakuwa na nagfasi kwenye kikosi cha kocha Manuel Pellegrini na kuuzwa kwake kunapunguza idadi ya wachezaji wa kigeni Manchester City.

Ameondoka: Javi Garcia ameuzwa kwa Pauni Milioni 13 Zenit St Petersburg


.png)
0 comments:
Post a Comment