• HABARI MPYA

    Friday, August 29, 2014

    ALONSO AKAMILISHA UHAMISHO WAKE BAYERN MUNICH KWA BEI KARIBU NA BURE

    KIUNGO Xabi Alonso amekamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 5 kutua Bayern Munich akitokea Real Madrid.
    Mchezaji huyo wa zamani wa Liverpool, alikuwa akihusishwa na mango wa kuhamia Manchester United baada ya miaka mitano ya kupiga kazi Bernabeu, lakini sasa anakwenda kuungana na Mspanyola mwenzake, kocha Pep Guardiola.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 32 anakwenda kwa mabingwa hao wa Ujerumani katika wakati ambao wanakabiliwa na majeruhi wengi, wakiwemo Javi Martinez, Bastian Schweinsteiger na Thiago Alcantara. 
    Salamu Munich: Xabi Alonso amejiunga na Bayern Munich akitokea Real Madrid kwa dau la Pauni Milioni 5Touch down: Former Liverpool man Alonso arrived in Munich ahead of his medical
    Anamwaga wino: Nyota wa zamani wa Liverpool, Alonso akiwasaini mashabiki mjini Munich wakati anakwenda kufanyiwa vipimo vya afya
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ALONSO AKAMILISHA UHAMISHO WAKE BAYERN MUNICH KWA BEI KARIBU NA BURE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top