NI Ujerumani. Ujerumani imetwaa ubingwa wa dunia, baada ya kuiangusha Argentina kwa bao 1-0 katika mchezo wa Fainali Uwanja wa Maracana mjini Rio de Jeneiro, Brazil.
Shukrani wake, Mario Gotze aliyeingia kuchukua nafasi ya Miroslav Klose dakika 88, aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 112.
Hilo linakuwa taji la nne la Kombe la Dunia kwa Ujerumani na sifa zimuendee kipa Manuel Neuer aliyeokoa mabao mengi ya wazi na kuwakatili Argentina walioongozwa na nyota wao, Lionel Messi.
Refa Nicola Rizzoli wa Italia alikataa bao la Gonzalo Higuain dakika ya 32 akimalizia krosi ya Lavezzi, kwa kuwa mchezaji huyo aliotea, ingawa tayari alikwishaanza kushangilia.
Kikosi cha Ujerumani kilikuwa; Neuer, Lahm, Boateng, Hummels, Howedes, Kramer/Schurrle dk32, Schweinsteiger, Muller, Kroos, Ozil, Klose/Gotze dk88.
Argentina: Romero, Zabaleta, Demichelis, Garay, Rojo, Biglia, Mascherano, Perez/Gago dk86, Higuain/Palacio dk78, Messi na Lavezzi/Aguero dk46.
Shukrani wake, Mario Gotze aliyeingia kuchukua nafasi ya Miroslav Klose dakika 88, aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 112.
Hilo linakuwa taji la nne la Kombe la Dunia kwa Ujerumani na sifa zimuendee kipa Manuel Neuer aliyeokoa mabao mengi ya wazi na kuwakatili Argentina walioongozwa na nyota wao, Lionel Messi.
Ujerumani wakishangilia na Kombe la baada ya mechi |
Shujaa; Mario Gotze akifunga bao la ubingwa |
Mario Gotze akishangilia baada ya kufunga bao la ushindi kwa Ujerumani |
Refa Nicola Rizzoli wa Italia alikataa bao la Gonzalo Higuain dakika ya 32 akimalizia krosi ya Lavezzi, kwa kuwa mchezaji huyo aliotea, ingawa tayari alikwishaanza kushangilia.
Kikosi cha Ujerumani kilikuwa; Neuer, Lahm, Boateng, Hummels, Howedes, Kramer/Schurrle dk32, Schweinsteiger, Muller, Kroos, Ozil, Klose/Gotze dk88.
Argentina: Romero, Zabaleta, Demichelis, Garay, Rojo, Biglia, Mascherano, Perez/Gago dk86, Higuain/Palacio dk78, Messi na Lavezzi/Aguero dk46.
0 comments:
Post a Comment