• HABARI MPYA

    Monday, July 21, 2014

    TAIFA STARS NA MAMBAS ZILIVYOONYESHANA KAZI JANA

    Mshambuliaji wa Tanzania, Mbwana Samatta akipasua katikati ya mabeki wa Msumbiji ambao walimchezea rafu na kusababisha penalti iliyofungwa na Khamis Mcha 'Vialli' kuipatia Taifa Stars bao la pili katika sare ya 2-2 na Mambas katika mchezo huo wa kwanza hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Morocco, uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.
    Mbwana Samatta akienda chini baada ya kuchezewa rafu na Zainadine Junior kulia
    Mfungaji wa mabao ya Stars jana, Khamis Mcha 'Vialli' kulia akitia krosi

    Mshambuliaji wa Stars John Bocco 'Adebayor' alibaki yeye na kipa Dario Khan akashindwa kufunga 

    John Bocco akiwatoka mabeki wa Msumbiji

    Mshambuliaji wa Taifa Stars, Mrisho Ngassa akiwalamba chenga mabeki wa Msumbiji

    Beki wa Tanzania, Oscar Joshua kulia akipambana na Benedicto Bernedicto wa Msumbiji

    Thomas Ulimwengu wa Taifa Stars akipiga krosi

    Kikosi cha Taifa Stars jana

    Kikosi cha Msumbiji jana

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS NA MAMBAS ZILIVYOONYESHANA KAZI JANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top