• HABARI MPYA

    Monday, September 18, 2017

    KOCHA NJOMBE MJI ANG’ATUKA BAADA YA KUPIGWA MECHI TATU MFULULIZO

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    TIMU ya Njombe Mji imepata pigo baada ya kocha wake Mkuu, Hassan Banyai kung’atuka kufuatia matokeo mabaya katika mechi tatu za mwanzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. 
    Njombe Mji FC imefungwa mechi zote tatu za mwanzo za Ligi Kuu, mbili nyumbani Uwanja wa Saba Saba dhidi ya Tanzania Prisons 2-0 na Yanga SC 1-0 kabla ya kuchapwa 1-0 na Mbeya City Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
    Na kabla ya kuingia kwenye mchezo wa nne dhidi ya Ruvu Shooting Septemba 23, mwaka huu, leo Njombe Mji imetoa taarifa ya kutengana na kocha wake aliyeipandisha timu Ligi Kuu msimu huu.
    Afisa Habari wa Njombe Mji FC, Solanus Mhagama amesema kwamba kwa kipindi hiki, aliyekuwa Kocha Msaidizi, Mrage Kabange ndiye ataiongoza timu hadi hapo uongozi utakapotoa tamko longine.
    Njombe Mji imemshukuru Banyai kwa mchango wake kwenye timu ikiwemo kuipandisha Ligi Kuu na kumtakia kila la heri huko aendako.
    Mhagama amesema kwa sasa wanaelekeza nguvu kwenye mchezo wao ujao dhidi ya Ruvu Shooting Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani mwishoi mwa wiki.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOCHA NJOMBE MJI ANG’ATUKA BAADA YA KUPIGWA MECHI TATU MFULULIZO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top