Beki Marcos Rojo akikimbia kushangilia kishujaa huku amedandiwa mgongoni na Nahodha wake, Lionel Messi baada ya kuifungia Argentina bao la ushindi dakika ya 86 ikiilaza Nigeria 2-1 katika mchezo wa mwisho wa Kundi D Kombe la Dunia leo Uwanja wa Saint-Petersburg nchini Urusi. Argentina ilitangulia kwa bao la Messi dakika ya 14, kabla ya Victor Moses kuisawazishia Super Eagles kwa penalti dakika ya 51, kufuatia Javier Mascherano kumshika hadi kumungusha Leon Balogun kwenye boksi wakati wa kona. Lakini refa Cuneyt Cakir aliingia lawamani kwa kuwanyima penalti ya pili Nigeria, huku Argentina ikienda hatua ya 16 Bora kama mshindi wa pili wa kundi kwa pinti zake nne nyuma ya Croatia, iliyomaliza na pointi tisa. Argentina itamenyana na Ufaransa Juni 30, wakati Croatia itamenyana na Denmark Julai 1 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
🏆 Champions League returns: all you need to know about the last 16
-
The UEFA Champions League enters its most exciting phase. After a draw that
resulted in matchups worthy of an early final, the 16 best teams on the
contine...
5 minutes ago



.png)
0 comments:
Post a Comment