• HABARI MPYA

    Saturday, January 16, 2016

    KIPYENGA CHA KWANZA CHAN 2016 LEO; NI RWANDA NA IVORY COAST

    Rwanda watamenyana na Ivory Coast leo katika mechi ya ufunguzi ya CHAN Uwanja wa Amahoro

    FILIMBI ya kwanza ya michuano ya nne ya Kombe la Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) inatarajiwa kupulizwa leo mjini Kigali, nchini Rwanda.
    Wenyeji, Amavubi wanatarajiwa kufugua dimba kwa kucheza na Ivory Coast Uwanja wa Amahoro, Kigali kuanzia Saa 10:00 jioni katika mchezo wa Kundi A.
    Mchezo huo utafuatiwa na mchezo mwingine wa kundi hilo kati ya Gabon na Morocco utakaoanza Saa 1:00 usiku.
    Kesho mechi za Kundi B zinatarajiwa kuendelea, mabingwa wa kwanza wa michuano hiyo, DRC wakimenyana na Ethiopia Uwanja wa Huye kuanzia Saa 10:00 jioni, kabla ya Angola kumenyana na Cameroon Uwanja wa Huye pia kuanzia Saa 1:00 usiku.
    Rwanda inakuwa nchi ya nne kupewa uenyeji wa michuano hiyo inayoshirikisha wachezaji wanaocheza Ligi za nchini mwao pekee baada ya Ivory Coast mwaka 2009, Sudan 2011 na Afrika Kusini mwaka juzi.
    Bingwa wa kwanza wa michuano hiyo inayozidi kupata msisimko kila mwaka alikuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), aliyefuatiwa na Tunisia na baadaye Libya.

    MAKUNDI CHAN 2016;
    Kundi A; Gabon, Ivory Coast, Morocco na Rwanda
    Kundi B; Angola, Cameroon, DRC na Ethiopia
    Kundi C; Guinea, Niger, Nigeria na Tunisia
    Kundi D; Mali, Uganda, Zambia na Zimbabwe

    RATIBA KOMBE LA CHAN 2016 RWANDA
    Januari 16, 2016
    Rwanda Vs Ivory Coast (Amahoro, Saa 10:00 jioni)
    Gabon Vs Morocco (Amahoro, Saa 1:00 usiku)
    Januari 17, 2016
    DRC Vs Ethiopia (Huye, Saa 10:00 jioni)
    Angola Vs Cameroon (Huye, Saa 1:00 usiku)
    Januari 18, 2016
    Tunisia Vs Guinea  (Nyamirambo, Saa 10:00 jioni)
    Nigeria Vs Niger (Nyamirambo, Saa 1:00 usiku)
    Januari 19, 2016
    Zimbabwe Vs Zambia (Rubavu, Saa 10:00 jioni)
    Mali Vs Uganda (Rubavu, Saa 1:00 usiku)
    Januari 20, 2016
    Rwanda Vs Gabon (Amahoro, Saa 10:00 jioni)
    Morocco Vs Ivory Coast (Amahoro, Saa 1:00 usiku) 
    Januari 21, 2016
    DRC Vs Angola (Huye, Saa 10:00 jioni)
    Cameroon Vs Ethiopia (Huye, Saa 1:00 usiku)
    Januari 22, 2016
    Tunisia Vs Nigeria (Nyamirambo, Saa 10:00 jioni)
    Niger Vs Guinea (Nyamirambo, Saa 1:00 usiku)
    Januari 23, 2016
    Zimbabwe Vs Mali (Rubavu, Saa 10:00 jioni)
    Uganda Vs Zambia (Rubavu, Saa 1:00 usiku)
    Januari 24, 2016
    Morocco Vs Rwanda (Amahoro, Saa 11:00 jioni)
    Ivory Coast Vs Gabon (Huye, Saa 11:00 jioni)
    Januari 25, 2016
    Ethiopia Vs Angola (Amahoro, Saa 11:00 jioni)
    Cameroon Vs DRC (Huye, Saa 11:00 jioni)
    Januari 26, 2016
    Guinea Vs Nigeria (Rubavu, Saa 11:00 jioni)
    Niger Vs Tunisia (Nyamirambo, Saa 11:00 jioni)
    Januari 27, 2016
    Zambia Vs Mali (Nyamirambo, Saa 11:00 jioni)
    Uganda Vs Zimbabwe (Amahoro, Saa 11:00 jioni)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIPYENGA CHA KWANZA CHAN 2016 LEO; NI RWANDA NA IVORY COAST Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top