ENGLAND imepata ushindi wa mabao 3-2 ugenini dhidi ya Sloveania mchezo wa Kundi E kufuzu Euro 2016 usiku huu.
Milivoje Novakovic alianza kuifungia Slovenia dakika ya 37 kabla ya Jack Wilshere kuisawazishia England dakika ya 57, hilo likiwa bao lake la kwanza kuifungia Three Lions.
Wilshere akaifungia tena England bao la pili dakika ya 73, kabla ya Nejc Pecnik kuisawazishia Slovenia dakika ya 84.
Shujaa wa mchezo wa leo alikuwa Wayne Rooney aliyeifungia England bao la ushindi dakika ya 86.
Kikosi cha Slovenia kilikuwa; Handanovic, Brecko, Ilic, Cesar, Jokic, Mertelj, Kurtic, Illcic/Birsa dk61, Kampl, Kirm/Pecnick dk72 na Novakovic.
England; Hart, Jones/Lallana dk46, Cahill, Smalling, Gibbs, Henderson, Wilshere, Delph/Clyne dk86, Townsend/Walcott dk74, Rooney na Sterling.
Wayne Rooney akishangilia baada ya kuifungia England bao la ushindi dakika ya 86 dhidi ya Slovenia usiku huu PICHA ZAIDI GONGA HAPA


.png)
0 comments:
Post a Comment