• HABARI MPYA

    Saturday, November 15, 2014

    SOLOMON KALOU APIGA MBILI PEKE YAKE TEMBO LA IVORY COAST LIKIITIMBA SIERRA LEONE 5-1 KUFUZU AFCON

    Solomon Kalou alifunga mawili
    TIMU ya taifa ya Ivory Coast imepata ushindi mono wa mabao 5-1 dhidi ya Sierra Leone jana katika mchezo wa kuwania kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.
    Mchezo huo ulioshuhudiwa na umati mkubwa wa watu Abidjan, ulifurahia mabao yaliyofungwa na nyota wao, Salomon Kalou mawili, Kolo Toure, Max Gradel na Gervinho.
    Bao la kufutuia machozi la Sierra Leone lilifungwa na Mustapha Bangoura aliyegongeana vizuri na Alhassan Kamara.
    Ushindi huo unawafanya Tembo hao wafikishe pointi tisa, moja nyuma ya vinara wa kundi lao, Cameroon ambao leo wanacheza na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), yenye pointi sita.
    Kikosi cha Sierra Leone kilikuwa: Solomon Zombo Morris, Alie Sesay, David Simbo, Mustapha Dumbuya, John Kamara, Lansana Kamara, Mohamed Kamara, Mustapha Bangura, Hassan Sesay, Sherif Suma na Alhassan Kamara
    Ivory Coast: Sylvain Gbohouo, Kolo Toure, Siaka Tiene, Ousmane Viera Diarassouba, Serge Aurier, Yaya Toure, Geoffroy Serey Die, Max Gradel, Salomon Kalou, Gervinho na Lacina Traore.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SOLOMON KALOU APIGA MBILI PEKE YAKE TEMBO LA IVORY COAST LIKIITIMBA SIERRA LEONE 5-1 KUFUZU AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top