• HABARI MPYA

    Monday, November 17, 2014

    MOTO, MOTO, MOTO...MASHABIKI WAWASHA MOTO NA KUUTUPIA UWANJANI HADI MCHEZO WA ITALIA NA CROATIA UKASIMAMISHWA

    ITALIA imelazimishwa sare ya kufungana bao 1- 1 na Croatia katika mchezo wa Kundi H kufuzu Euro 2016, ambao ulilazimika kusimama kwa dakika 10 baada ya mashabiki kurusha vipeperushi vya moto Uwanja wa San Siro. 
    Wachezaji walitolewa nje dakika ya 75 baada ya mashabiki wa ugenini kutupia vipeperushi vya moto Uwanja wa San Siro, lakini hali ilitulia baada ya dakika 10 minutes na mchezo ukaendelea.
    UEFA inatarajiwa kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo kabla ya kuchukua hatua. Antonio Candreva alitangulia kuifungia Italia dakika ya 11, kabla ya Ivan Perisic kusawazisha dakika nne baadaye. Kiungo wa Real Madrid, Luka Modric alitolewa nje dakika ya 28 baada ya kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Mateo Kovacic.
    Kikosi cha Italia kilikuwa; taly: Buffon, Ranocchia, Chiellini, Darmian, De Rossi, Candreva, Pasqual/Soriano dk28, De Sciglio, Marchisio, Zaza/Pelle dk63 na Immobile/El Shaarawy dk52.
    Croatia: Subasic, Srna, Corluka, Vida, Pranjic, Modric/Kovacic dk28, Brozovic/Badelj dk83, Olic/Kramaric dk69, Rakitic, Perisic na Mandzukic.

    Flares are let off in the stand by Croatia fans, before being thrown on to the pitch and riot police arrived to calm things down

    Italy's Mattia De Sciglio (left) jumps to compete for the ball against Croatia's Darijo Srna on Sunday
    Mattia De Sciglio wa Italia (kushoto) akiruka juu kugombea mpira na Darijo Srna wa Croatia jana

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2836967/Italy-1-1-Croatia-European-Championship-qualifier-suspended-10-minutes-second-half.html#ixzz3JIj7Vef5 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MOTO, MOTO, MOTO...MASHABIKI WAWASHA MOTO NA KUUTUPIA UWANJANI HADI MCHEZO WA ITALIA NA CROATIA UKASIMAMISHWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top