• HABARI MPYA

    Friday, August 15, 2014

    WEST HAM YASAJILI STRAIKA LA SENEGAL LILILOTISHA KWA MABAO UFARANSA

    KLABU ya West Ham imeimarisha safu yake ya ushambuliaji kwa kumsajili Diafra Sakho kutoka FC Metz ya Ufaransa.
    The Hammers imetangaza katika tovuti yake kwamba mpachika mabao huyo mwenye umri wa miaka 24 amesaini mkataba wa miaka minne, ingawa dau halikutajwa.
    Mchezaji huyo wa Senegal anahamia England baada ya kung'ara Metz, akifunga mabao 43 katika misimu miwili iliyopita na kuiwezesha klabu hiyo kurejea Ligi Kuu.
    Dili limetiki: West Ham imekamilisha usajili wa Diafra Sakho  kutoka Metz ya Ufaransa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WEST HAM YASAJILI STRAIKA LA SENEGAL LILILOTISHA KWA MABAO UFARANSA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top